,

Mafanikio Quotes

Quotes tagged as "mafanikio" Showing 1-30 of 31
“Wakati mwingine kufukuzwa kazi ni kama kujengewa ukuta kwenye njia upitayo hata hivyo wakati mwingine ni namna ya kupata uelekeo sahihi.”
Suzy Kassem, Rise Up and Salute the Sun: The Writings of Suzy Kassem

Enock Maregesi
“Ukitaka kufanikiwa katika maisha angalia watu wanataka nini halafu wape. Kama wanataka burudani wape. Kama wanataka elimu wape. Kama wanataka bidhaa wape. Kama wanataka huduma wape. Wape kwa msaada wa wataalamu.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kuna ndoto za mchana na kuna ndoto za usiku. Ndoto za mchana ni maono ya kile ambacho roho inatamani kuwa. Ndoto za usiku ni maono yanayotokea wakati akili imetulia baada ya mwili wote kupumzika. Ukiota kuhusu moto, hiyo ni ishara ya hasira; ukiota kuhusu maji, hiyo ni ishara ya siri; ukiota kuhusu ardhi, hiyo ni ishara ya huzuni; ukiota kuhusu Yesu, hiyo ni ishara ya mafanikio. Kitu cha kwanza kufanya unapoota ndoto za kishetani, utakapoamka, mwombe Mungu akunusuru kutoka katika matatizo yoyote yanayokunyemelea; au yanayomnyemelea mtu mwingine yoyote yule, hata usiyemjua. Ubongo ni kitu cha ajabu kuliko vyote ulimwenguni na umetengenezwa na Mungu. Ndoto zinapatikana ndani ya ubongo. Ubongo unapatikana ndani ya ufahamu. Ufahamu mtawala wake ni malaika mwema. Malaika mwema anajua siri ya ndoto. Kila mtu anaota na kila ndoto ina maana yake. Rekodi ndoto zako kila siku kwa angalau mwezi mzima kupata maana halisi ya ndoto hizo, na kujua kwa nini ulizaliwa.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kufanikiwa katika maisha lazima kitu fulani ambacho si cha kawaida kitokee katika maisha yako, bila kujali uko upande wa Yesu au upande wa Shetani. Kufanikiwa katika maisha ni sawa na kwenda mbinguni, au kuishi mbinguni duniani. Kitu ambacho si cha kawaida kutokea katika maisha yako ni sawa na kifo. Fanya kitu ambacho hujawahi kufanya kupata kitu ambacho hujawahi kupata.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Siri ya mafanikio yako ni chumba chako. Dali linasema anga ndicho kipimo cha kufikiria; Dirisha linasema utazame nje uone fursa zilizopo ulimwenguni; Feni linasema uwe mtulivu usikurupuke kufanya lolote; Kalenda inasema uwe mtu anayekwenda na wakati; Kioo kinasema ujitazame na ujiamini kabla ya kutenda lolote; Kitabu cha dini kinasema unapaswa kumwamini Mungu ili uishi; Kitanda kinasema ujifunze kuwa na likizo; Mlango unasema usipitwe na fursa ya aina yoyote ile hapa duniani; Saa inasema kila sekunde ina thamani sana katika maisha yako hivyo tumia muda wako vizuri. Amka uishi.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mungu akikubariki kipaji chako watu watasema ni laana. Maisha yako ni sawa na mto. Unakoelekea ni baharini. Lakini sasa umefika kwenye mlango wa bahari. Unahangaika upite wapi kufika baharini, ambapo utaogelea kwa kadiri utakavyoweza. Utakapofika baharini, watu, badala ya kusema umebarikiwa, watasema umelaaniwa, badala ya kukuita malaika, watakuita shetani. Mafanikio hayapimwi kwa pesa au mali kiasi gani unayo, mafanikio yanapimwa kwa amani ya moyo au maisha ya watu kiasi gani umeboresha.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukitaka kutambulika usione aibu.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“The biggest barrier in success is the nightmare – You will have to endure the nightmare to be successful.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Wakati mwingine tukitaka kufanikiwa lazima tujifunze kutunza siri.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kutunza siri wakati mwingine ni kitu kigumu sana kwa baadhi ya watu lakini watu wanapaswa kuwa na uwezo wa kutunza siri kujijengea uaminifu, ambao ni siri ya mafanikio.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Nyota ni kipaji, kipawa, takdiri, karama, au uweza; ni kiashiria cha rohoni kinachoonyesha mtu atakuwa nani baadaye, mafanikio ya mtu, au takdiri ya maisha ya mwanadamu. Unabii na nyota ya ufalme ni kibali cha Mungu katika maisha ya mtu. Kupata kibali hicho, tembea na watu sahihi katika maisha yako (tembea na watu ambao Mungu amekuchagulia kushika funguo za takdiri ya maisha yako). Tamka na kukiri kibali cha Mungu katika maisha yako yote. Panda mbegu za kibali cha Mungu katika udongo wa maisha yako. Jifunze kutenda mema bila malipo, kwani wema ni mbegu ya kibali cha Mungu. Jali mambo ya ufalme wa Mungu.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mafanikio unapaswa kuyataka kama unavyotaka hewa. Hewa ni kitu cha muhimu zaidi kuliko kitu kingine chochote kile ulimwenguni. Ukipewa hewa au shilingi bilioni kumi chagua hewa.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kuna mafanikio ya aina mbili hapa duniani: Mafanikio ya Shetani na mafanikio ya Mungu. Mafanikio ya Shetani ni rahisi kupata na ni ya kitumwa. Mafanikio ya Mungu ni magumu kupata lakini ni ya hakika. Mungu akikubariki, pesa inaongezeka kama inavyoongezeka saa.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukiwa na mafanikio ya Shetani hayo si mafanikio ya kweli. Ukiwa na mafanikio ya Mungu hayo ndiyo mafanikio ya kweli. Mafanikio ya kweli hayatokani na NINI unacho. Mafanikio ya kweli yanatokana na NANI unaye. Yesu Kristo alikuwa maskini, hakuwa na kitu; lakini alikuwa tajiri, alikuwa na Mungu ndani ya moyo wake.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Aidha, tunaweza kupata inkishafi kutokana na asili ya miili yetu, matukio fulani ya wakati ujao yana asili yake katika ndoto za binadamu. Ndoto hizo au maono hayo ni ishara ya kile kinachokuja mbele katika maisha ya mtu; kama vile afya, ugonjwa au hatari. Ukiota kuhusu moto, hiyo ni ishara ya hasira – unatakiwa kuwa na hekima; ukiota kuhusu mimba na unajifungua, hiyo ni ishara ya kuwa katika mchakato wa kutengeneza wazo jipya – unatakiwa kushukuru; ukiota unaruka angani, hiyo ni ishara ya tumaini – unatakiwa kushukuru; ukiota kuhusu maji au kiowevu kingine chochote kile, hiyo ni ishara ya siri na wakati mwingine ni ishara ya kuwa na matatizo ya kiafya kama utaota kuhusu maji machafu – unatakiwa kuwa msiri na msafi; ukiota kuhusu ardhi, hiyo ni ishara ya huzuni – unatakiwa kuomba; na ukiota kuhusu Yesu, hiyo ni ishara ya mafanikio – unatakiwa kushukuru.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kama huna mama, kama mama yako alishafariki, au kama yupo lakini hakujali, hata kama baba yako yupo au hayupo, mafanikio yako yatatokana na juhudi zako mwenyewe.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Damu ya Mwanakondoo ina nguvu kuliko maombi. Mungu hauwi, Anamtumia Shetani kama wakala wake wa kutoa adhabu kwa binadamu. Ukifunikwa na damu ya Mwanakondoo Shetani, ambaye ni wakala, hatakuona. Lakini Mungu atakuona. Bila kafara ya damu hakuna msamaha wa dhambi. Bila kafara ya damu hakuna mafanikio.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukifuata kanuni ya nguvu ya uvutano uhitaji kujua jinsi utakavyofanikiwa. Kazi yako ni kuwaza tu kwa namna inavyotakiwa. Waza na amini kwa asilimia mia moja. Mengine yote mwachie Mungu au ulimwengu. Mungu pekee ndiye anayekupa njia na bahati, ili wewe ufanikiwe. Atakupa nguvu ya kufanya kazi na ujanja wowote utakaohitajika, katika harakati hizo za mafanikio yako.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukiwaza kwa kufuata kanuni ya nguvu ya uvutano (ambayo ni kuwaza na kuamini kama kile unachokiwaza tayari umeshakipata bila hata kujua umekipataje) utaishi kama ulivyowaza. Ukiwaza kuwa jambazi utakuwa jambazi hakika, ukiwaza kupona ugonjwa unaokusumbua utapona hakika, na ukiwaza kuwa tajiri utakuwa tajiri hakika. Mafanikio hayo yanaweza kuchukua mwezi mmoja kutimia au yanaweza kuchukua miaka kumi. Unachotakiwa kufanya ni kuwaza na kuamini.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Amani ya moyo ndicho kipimo cha mafanikio yetu.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kuwa teja wa mafanikio.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kuwa na uraibu wa mafanikio, si wa dawa.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukikaa nyuma yangu utafanikiwa, ukikaa mbele utaanguka.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Siri ya mafanikio ni shida!”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Maisha yangu ni kafara ya mafanikio yangu.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mafanikio ni matokeo mazuri ya jambo lolote na ni tofauti kwa kila mtu. Kama ulivyo uzuri, mafanikio yapo katika macho ya aonaye. Ni jukumu lako kujua mafanikio yana maana gani kwako, na jinsi gani umeyapata mafanikio hayo.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kufika hapa nilipofika leo nilijitolea vitu vingi na mambo mengi katika maisha yangu. Niliishi katika uhamisho wa kijamii kwa ajili ya mafanikio. Nilijitolea muda. Nilijitolea usingizi. Nilijitolea starehe. Wakati wengine wakienda baa mimi nilikuwa kazini. Wakati wengine wamelala, mimi nilikuwa macho nikifanya kazi. Wakati wengine wakiangalia vipindi pendwa vya televisheni, mimi nilikuwa nikiangalia vipindi visivyopendeka vya televisheni. Wakati wengine wana muda wa kuchezea, mimi nilikuwa nikiyaendesha maisha yangu kwa ratiba maalumu.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Unataka kufanikiwa lakini hutaki watu wakuone. Kama una kipaji kionyeshe kwa watu.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukiwa juu uwezekano wa kushuka chini ni mkubwa sana, kuliko ukiwa chini ambapo uwezekano wa kupanda juu ni mkubwa sana.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kuna siri nyingi za ndani zinazofanya mtu aendelee kufanikiwa, na kuna siri nyingi za nje zinazofanya mtu aendelee kuficha siri ya mafanikio yake. Siri za ndani ni siri za kweli, ilhali siri za nje ni siri za uongo, zenye lengo la kuficha ukweli. Hata hivyo, siri ya mafanikio ni kufanya kazi kwa bidii na maarifa, pamoja na siri.”
Enock Maregesi

« previous 1