,

Mungu Quotes

Quotes tagged as "mungu" Showing 1-30 of 194
“Sijafika. Ndio maana simdharau MTU wala hassle yake. Na nitakapofika, bado nitakumbuka Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kupeana riziki.”
DON SANTO

Enock Maregesi
“Palestina ni nchi ya Waisraeli waliyopewa na Mungu wa Yakobo. Hata hivyo, hawakutimiza masharti. Mungu aliwaagiza kuua kila mtu katika nchi ya Kaanani na miji yake yote. Waisraeli, wakiongozwa na Yoshua, waliua watu wengi katika nchi ya Kaanani. Hawakuua kila mtu katika miji ya Ashdodi, Gathi na Ukanda wa Gaza kama walivyoagizwa. Mungu alimwambia Ibrahimu kuwa angempa yeye na uzao wake nchi ya Kaanani kuwa milki yao ya milele, na kuwa Yeye ndiye angekuwa Mungu wao daima. Vita ya Israeli na Palestina itamalizwa na Mungu. Itamalizwa na hekima.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mungu alikupa maisha akakupa akili ili utambue jema na baya na akakupa amri zake ili uishi kwa amani na upendo. Kama Mungu hayupo mwanamume na mwanamke walitoka wapi? Wazazi wako walitoka wapi? Wazazi wao walitoka wapi? Wazazi wao walitoka wapi?”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mungu hagawi pesa kwa watu kama watu wanavyofikiria. Anagawa upendo na hekima.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kama Mungu na Shetani hawako ndani yako, hiyo vita ya kiroho unaipigania wapi?”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Baraka inapotoka kwa Mungu lengo lake ni kukufanya umpende Mungu kupitia wenzako.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Heshimu kila mtu. Ongea na kila mtu. Msikilize kwa makini kila unayeongea naye. Maana Mungu anaweza kumtumia mtu yeyote, hata kichaa, kukupa ufunuo wa mambo yake.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kuna watu hawaamini kama Mungu yupo, lakini maisha yao yanaamini.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mungu asingekuwepo matajiri wangehonga kifo ili waishi milele.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Watoto wadogo wanakufa. Watu wazima wasiokuwa na hatia wanakufa vitani na katika majanga mengine ya asili. Kwa nini? Watoto wadogo wanaokufa walikuja duniani kufanya nini? Kwa nini watu wasiokuwa na hatia wanakufa ilhali Mungu yupo na asiwaepushe na matatizo ya dunia hii? Kama aliweza kuzuia binadamu wasiishi majini kwa sababu watakufa kwa nini asizuie matatizo yasiwapate watoto na watu wazima wasiokuwa na hatia? Sisi ni wadogo sana na Mungu ni mkubwa mno. Jibu hatutaweza kulielewa pamoja na kwamba tumepewa. Hata hivyo, Mungu hababaishwi na mwili. Anababaishwa na roho.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Adamu na Hawa walipotenda dhambi waligundua kuwa kumbe walikuwa na miili, walipogundua kuwa walikuwa uchi, kisha Mungu akawalaani. Miili yao ikakosa thamani mbele ya Mungu, sisi wote tukalaaniwa pamoja nao. Kwa Mungu hii miili haina thamani hata kidogo. Chenye thamani ni roho.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mungu angekuwa anababaishwa na mwili asingeruhusu Shetani autese mwili wa Ayubu kiasi chote kile isipokuwa roho yake, wala tusingekuwa tunateseka, wala watoto wadogo wasingekuwa wanakufa, wala watu wasiokuwa na hatia wasingekuwa wanakufa vitani au katika majanga mengine yoyote yale katika dunia hii.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mitume wa Yesu Kristo wakati wanahubiri injili hawakuwa na Roho Mtakatifu, walikuwa hata bado hawajaongoka, lakini walikuwa na idhini maalumu kutoka kwa Mungu ya kuhubiri Neno la Mungu. Neno la Mungu halihubiriwi kwa nguvu zetu sisi wenyewe bali linahubiriwa kwa nguvu za Mungu kutokana na utii kwa uongozi wake.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Utii kwa Mungu unapokosekana injili ambayo Mungu anataka ihubiriwe haitahubiriwa. Itahubiriwa na manabii wa uongo.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Jukumu la kwanza la kanisa ni kueneza injili duniani kote kama tunavyoambiwa katika mathayo 24:14. Haijalishi utaieneza vipi, kwa sababu Mungu hajasema tuieneze vipi. Lakini la kwanza kabisa ni kuwa kwanza mwaminifu kwa Mungu kuweza kueneza injili duniani kote.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mungu ni mkubwa kuliko jumla ya matatizo yote na vitu vyote alivyoviumba na ana uwezo wa kufanya kila kitu alichosema atafanya bila kupunguza au kuongeza chochote. Usidanganywe na matatizo. Amka, kabla kifo hakijakufika.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Licha ya matatizo yanayotokea tunapaswa kujua kwa imani kwamba Mungu asiyeonekana na mwenye nguvu bado yuko kwenye kiti chake cha enzi, akisimamia kila kitu kinachoendelea, huku akijua bayana kwamba mapenzi yake lazima yatimie, bila kujali watu wasiomwamini wenye upofu wa rohoni.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mtu anayejaribu kupambana na Mungu anajaribu kupambana na jambo lisilowezekana. Hatakuwa na uwezo wa kushinda. Kufanya hivyo ni upumbavu usioweza kuelezeka, lakini wanadamu hatukomi kufanya hivyo.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Watu wote ni wa Mungu, watu ni matatizo. Wewe huna mtu, lakini bado unapambana na Mungu kuhusu watu.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Matatizo tunayopitia si matatizo kwa ukuaji wetu. Mungu hafanyi hivyo eti kutukomoa. Anafanya hivyo kwa faida yetu ya baadaye.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kinachosababisha tupambane na Mungu ni matatizo, ambayo huletwa na watu, na tunapambana kwa silaha ya uongo.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kuwa na kiasi katika matarajio yako. Hatuna uwezo wa kuona mambo kama Mungu anavyoyaona.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Wenye mamlaka wana dhamana za mamlaka zao kama watumishi wa Mungu, kwa sababu Neno la Mungu liko wazi kwamba Mungu ndiye aliyewapa mamlaka hayo.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukimheshimu baba au mama yako katika mambo mema au mabaya umemheshimu Mungu katika mambo mema.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kama miaka 1000 ya duniani ni sawa na siku moja ya Mungu; hivyo basi, miaka 930 aliyoishi Adamu ni sawa na siku 0.93 au saa 22:32 za Mungu. Kwa hiyo, ili siku ya Mungu itimie Adamu alipaswa kuishi miaka 70 (siku 0.07 au saa 1:68) zaidi! Ukiidadavua saa 1:68 unapata saa 2:08. Kulingana na muda wa mbinguni tunapaswa kuishi kwa muda wa saa 2:08! Muda huo ni mfupi sana.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kulingana na muda wa Mungu, maisha ya Adamu yalikuwa siku 0.93 au saa 22:32! Maisha ya mwanadamu ni siku 0.07 au saa 1:68!”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukijidharau unadharau uwezo ambao Mungu alikuwekea ndani yako.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukila kiapo cha uaminifu, kwa mfano, kwa jina la Mwenyezi Mungu, kisha uaminifu huo ukakushinda, nini kitatokea? Laana! Yaani, badala ya kubarikiwa, utalaaniwa na Mungu.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Anza. Mungu mwenyewe atakuonesha njia.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Tanzania ina majanga mawili kuhusiana na UVIKO-19: Janga la Korona na janga la watu wasiotaka kuchanjwa! Nisikilize! Kataa kwa hekima! Acha Mungu achanjwe kwa niaba yako!”
Enock Maregesi

« previous 1 3 4 5 6 7