Nenda kwa yaliyomo

Muziki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Wanamuziki)
Zumari kutoka miaka 41,000 iliyopita iliyotengenezwa kwa mfupa.
Mchoro wa Ugiriki wa Kale juu ya chombo ukionyesha kipindi cha muziki (510 KK hivi).

Muziki ni mpangilio wa sauti ili kuunda mseto wa umbo, utangamano, melodi, mdundo, au vilevile mbinu elezi. Muziki kwa ujumla unakubaliwa kuwa utamaduni wa ki-ulimwengu na hupatikana katika jamii zote za wanadamu.

Ufafanuzi wa muziki hutofautiana sana kifalsafa na kimbinu. Ingawa wasomi wanakubali kwamba muziki unafafanuliwa na vipengele maalum, hakuna makubaliano kuhusu uhakika wa vipengele hivi. Mara nyingi, muziki hutambulishwa kama mbinu ainati ya kuwasilisha ubunifu. [1]

Shughuli mbalimbali huhusika katika uundaji wa muziki, na mara nyingi hugawanywa katika kategoria za utunzi, ubunifu tendi na uigizaji. Muziki unaweza kuimbwa kwa kutumia ala mbalimbali za muziki, ikiwemo sauti ya binadamu. Inaweza pia kutungwa, kupangwa, au kuchezwa kifundi au kielektroniki, kama vile kisanduku muziki, paipu bareli, au programu dijitali kwenye kompyuta.

Muziki ni aina ya sanaa inayotumia sauti mbalimbali: za kibinadamu na za ala za muziki, ama kwa pamoja au kila moja pekee.

Asili ya neno iko katika lugha ya Kigiriki ambamo huitwa μουσική (mousikee).

Baadhi ya sifa za muziki ni uzito wa sauti (pitch) na wizani au mahadhi (rhythm).

Aina ya muziki inayopatikana kote duniani ni nyimbo ambazo ni maneno yanayotolewa kwa sauti na mahadhi fulani mara nyingi pamoja na ala za muziki. Kwa wanaorekodi sauti, wao huenda kwa studio kurekodi na huchukuliwa kwa kinasasauti kilichoambatanishwa na tarakilishi na kudhibitiwa na kompresa.

Wanamuziki maarufu wa Afrika

[hariri | hariri chanzo]

Wanamuziki maarufu wa Ulaya

[hariri | hariri chanzo]
  1. Hoad, T. F., ed. (2003). "music". The Concise Oxford Dictionary of English Etymology. ISBN 978-0-19-283098-2 . https://www.oxfordreference.com/view/10.1093/acref/9780192830982.001.0001/acref-9780192830982-e-9933. Retrieved 30 May 2022.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya muziki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Muziki kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.